1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

1860 Munich yakabiliwa na hali mbaya ya fedha

Sekione Kitojo
1 Juni 2017

Mabingwa  wa  zamani wa  ligi  ya  Ujerumani  Bundesliga 1860 Munich  wamesema  mfadhili  wake mkuu Hasan Ismaik  ameweka masharti  kwa  timu  hiyo  ambayo  hayawezi  kutimizwa

https://p.dw.com/p/2dzoV
Fußball 1860 Muenchen gegen Jahn Regensburg - 2. Bundesliga Playoff Leg 2
Wachezaji wa 1860 Munich iliyoteremka daraja la tatu nchini UjerumaniPicha: Getty Images/Bongarts/A. Hassenstein

Hali  hiyo  ya  mkwamo  inahatarisha  hatima  ya  klabu  hiyo wakati  muda maalum uliowekwa  na  shirikisho  la  soka  la  Ujerumani DFB kulipa  fedha  kwa  ajili  ya  leseni ya kucheza  katika  daraja  la  tatu  ukikaribia.

1860 ambayo  ilishishwa  daraja  kutoka  daraja  la  pili nchini Ujerumani  Jumanne  iliyopita  na  kuelekea  katika  daraja  la  tatu , inakabiliwa  na  kufilisika  na  kushushwa  hadi  daraja  la  nne  ama la  tano  hadi  pale  itakapoweza  kulipa  chama  cha  kandanda  cha Ujerumani  liseni  yake  ya  daraja  la  tatu ifikapo Ijumaa  mchana.

Makamu  wa  rais Heinz Schmidt  na  Hans Sitzberger wanasema katika  taarifa  kwamba "kabla ya  mchezo  wa  mchujo", Ismaik alikuwa  tayari  ameeleza  nia  yake ya  kuisaidia  timu  hiyo  kifedha , bila  kujali ni  ligi  gani  timu  hiyo  itacheza, katika  idadi  kadhaa  ya madai  ambayo  klabu  haiwezi kuyatimiza kwa  sababu  za  kisheria na  kiutawala. Taarifa kutoka  kwa  chama  cha  kandanda  zinaunga mkono  tathimini  yetu,  wamesema.