1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Adhabu ya kifo yazuwiliwa angalao kwa sasa Florida na Kalifornia

16 Desemba 2006
https://p.dw.com/p/CCiu

Washington:

Majimbo ya Marekani ya Florida na California yameamua kusitisha utekelezaji wa hukumu ya kifo.Watu wawili waliokua wauliwa kwa kudungwa sindano ya sumu katika majimbo yote hayo mawili walitaabika kwa muda mrefu hadi walipokata roho.Mhukumiwa katika jimbo la Florida alitaabika kwa nusu saa nzima jumatano iliyopita kwasababu sindano ya sumu alidungwa sivyo.Kisa kama hicho kilijiri pia Kalifornia mwaka jana.Korti kuu ya katiba inapiga marufuku watu kuuliwa kinyama kama hivyo.