1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

AFCON: Cameroon yaingia fainali

3 Februari 2017

Cameroon imeichapa Ghana mabao mawili kwa bila na kujihakikishia nafasi katika fainali ya kombe la mataifa ya Afrika AFCON. Cameroon itakuwa inawania ubingwa kwa mara ya tano itakapopambana na Misri.

https://p.dw.com/p/2WuBC
Michael Ngadeu-Ngadjui wa Cameroon
Picha: Reuters/A. Abdallah Dalsh

Michael Ngadeu-Ngadjui aliutikisa wavu wa Ghana katika dakika ya 72 kwa kufunga bao la kwanza na dakika tatu kabla ya kipenga cha mwisho Christian Bassogog aliyamaliza mashaka yote kwa kuifungia bao la pili timu yake ya Cameroon. Ghana na Burkina Faso zitapambana Jumamosi kuwania nafasi ya tatu. Fainali itachezwa Jumapili katika mji wa Libreville, Gabon.