1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Amman. Abbas anasema matumaini bado yako kwa mazungumzo ya serikali ya umoja.

15 Oktoba 2006
https://p.dw.com/p/CD2X

Rais Mahmoud Abbas ameeleza masikitiko yake leo kwa kuendelea hali ya mgawanyiko baina ya chama chake cha Fatah na Hamas , akisema kuwa bado kuna nafasi ya mazungumzo ya kuunda umoja.

Chama cha Hamas kinaongoza serikali ya nchi hiyo baada ya ushindi wa kishindo wa bunge mwezi wa januari.

Msaada wa kimataifa wa fedha katika mamlaka hiyo ya Wapalestina umesitishwa kutokana na chama cha Hamas kushindwa kutangaza kujiweka mbali na matumizi ya nguvu pamoja na kuitambua Israel kuwepo.