1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

AMSTERDAM: Kuelekea kuundwa serikali ya muungano

24 Novemba 2006
https://p.dw.com/p/CCpu

Matokeo ya uchaguzi nchini Uholanzi hayajakamilisha muelekeo wa kisiasa baada ya vyama mashuhuri kushindwa kupata wingi wa viti kuweza kulidhibiti bunge. Chama cha waziri mkuu, Jan Peter Balkenende cha Christian Demokratik, kimeonekana kuwa mshindi kwa kunyakua viti 41juu ya viti 150 vinavyowaniwa katika baraza la wawakilishi. Lakini kutokana na hali kwamba chama kikubwa cha upinzani cha Leba kilipata viti 32 na chama cha Socialist kupanda kutoka viti 9 hadi viti 26, haijaonesha mnamna itakavyoundwa serikali ya mseto. Wadadisi wa maswala ya kisiasa wamesema, kusamabaratisha kura na uungwaji mkono unaozidi kupanda kwa vyama vidogo vidogo vya kisiasa, kutapelekea kurefusha mazungumzo kwa ajili ya uundwaji wa serikali ya muungano.