1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

ATHENS: Wapigakura Ugiriki wachagua bunge jipya

16 Septemba 2007
https://p.dw.com/p/CBPM

Kiasi ya Wagiriki milioni 10 hii leo wanapiga kura kuchagua bunge jipya.Uchaguzi huu uliitishwa mapema na Waziri Mkuu Costas Karamanlis mwanzoni mwa mwezi wa Agosti,wakati ambapo chama chake cha kihafidhina „New Democracy Party“ kilikuwa kikiongoza.

Lakini uchunguzi wa maoni unaonyesha kuwa uchaguzi wa leo utakuwa mchuano mkali kati ya serikali na chama cha upinzani cha wasoshalisti PASOK,baada ya serikali kulaumiwa uongozi mbaya wakati wa maafa ya moto hivi karibuni.