1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BAGHDAD.Marekani yajenga ukuta kuwatenganisha wairak

22 Aprili 2007
https://p.dw.com/p/CC8A

Marekani imeanza kujenga ukuta utakaozitenganisha jamii za wasuni na washia katika mji mkuu wa Irak, Baghdad.

Msemaji wa jeshi la Marekani ameeleza kuwa ukuta huo wa kilometa 5 unajengwa ili kuimarisha usalama katika sehemu ambayo imekuwa inashambuliwa mara kwa mara.

Viongozi wa sehemu ambapo ukutwa utajengwa wamelalamika, lakini jenerali mmoja wa Irak amesema lengo la kujenga ukuta huo ni kuwazuia magaidi kufanya mashambulio.