1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Balozi wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo nchini Angola

22 Februari 2008

Kulingana na ripoti ya tume ya umoja wa mataifa nchini DRC, MONUC ni kwamba zaidi ya watu laki moja ambao ni raia wa Kongo walifukuzwa katika hali isiyo ya kibinaadamu nchini Angola katika kipindi cha mwaka mmoja.

https://p.dw.com/p/DBvP
Hali hiyo ilisababisha uhusiano baina ya Kongo na Angola kuzorota. Akiwa mjini Kinshasa balozi wa Kongo nchini Angola Bw.Paluku Shamavu ameelezea hali ya uhusiano kwa sasa baina ya nchi mbili hizo. Kwenye mahojiano na mwandishi wetu Saleh Mwanamilongo, balozi Paluku amezungumzia kwanza mategemeo walionayo kuhusu kongamano la Kidiplomasia kwa ajili ya DRC linalofanyika mjini Kinshasa.