1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Baraza la Usalama la UM kuiwekea vikwazo Sudan Kusini

Sekione Kitojo
1 Desemba 2016

Marekani inahangaika kuweza kupata idadi ya kutosha ya kura zinazohitajika kwa ajili ya baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa  kuweka vikwazo  dhidi ya Sudan Kusini.

https://p.dw.com/p/2TZfW
Südsudan Juba SPLA-IO Soldaten
Picha: picture-alliance/AP Photo/J. Patinkin

Marekani inahangaika kuweza kupata idadi ya kutosha ya kura zinazohitajika kwa ajili ya baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa  kuweka vikwazo dhidi ya Sudan Kusini huku Umoja wa Mataifa ukionya kuhusu uwezekano wa mauaji wa kimbari katika taifa  hilo  jipya duniani.

Azimio hilo linahitaji kura tisa na bila kupingwa kwa kura ya turufu ili kuweza kupitishwa, lakini wanadiploamsia waandamizi  wa  Umoja wa Mataifa, wakizungumza kwa masharti ya kutotajwa majina, wamesema hadi sasa ni wajumbe saba tu wanaokubali mswada  huo, wakati wajumbe wanane waliobaki wanapanga kujitoa kupiga kura ama kupiga kura ya hapana.

Wakati Urusi na China zina wasiwasi juu ya iwapo kuweka vikwazo vya silaha kunaweza kufikia hali ya amani wakati nchi hiyo  imetapakaa  silaha, wanadiplomasia hawatarajii nchi hizo kuzuwia hatua hiyo iwapo itafikishwa katika baraza hilo kupigiwa  kura.

Wanadiplomasia hao wamesema kuna matumaini kwamba Malaysia, Japan, Senegal na Angola zinaweza kushawishiwa kupiga  kura kuidhinisha azimio hilo badala ya kujizuwia kupiga kura iwapo mswada huo utapigiwa kura.