1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Bayern yakwaa kisiki

29 Oktoba 2012

Mtafaruku mkubwa wazuka katika pambano kati ya Manchester United na Chelsea katika permier League Jumapili(28.10.2012) refa atuhumiwa kuwauma Chelsea na pia kutoa matamshi ya kibaguzi dhidi ya wachezaji .

https://p.dw.com/p/16Yxn
MUNICH, GERMANY - OCTOBER 27: (L-R) Jerome Boateng and Claudio Pizarro of Bayern look dejected after losing 1-2 the Bundesliga match between FC Bayern Muenchen and Bayer 04 Leverkusen at Allianz Arena on October 27, 2012 in Munich, Germany. (Photo by Christof Koepsel/Bongarts/Getty Images)
Wachezaji wa FC Bayern Muenchen - wakiwa hoi baada ya kulazwa na Bayer 04 LeverkusenPicha: Bongarts/Getty Images

Maamuzi yasiyoridhisha pia yalitokea katika mpambano wa watani wa jadi Everton na Liverpool na Bayern Munich yaonja chungu ya kupigwa mwereka katika bundesliga, wakati mabingwa Borussia Dortmund na Schalke 04 baada ya ushindi mnono katika Champions League , zang'ara.

FC Bayern imekwaa kisiki wiki hii, pale mfululizo wake wa ushindi katika michezo minane ya Bundesliga ulipopigwa full stop na Bayer Leverkusen katika mchezo uliofanyika jana jioni. Bayern iliangukia pua baada ya kukubali kipigo cha mabo 2-1, na kuvutwa shati katika mbio zake katika uongozi wa ligi hiyo.

Hata hivyo Bayern inaendelea kuongoza ligi hiyo ikiwa na points 24 ikifuatiwa na Schalke 04 ambayo ina points 20. Mabao ya Stefan Kiessling na bao la kujifunga wenyewe la Jerome Boateng yalihakikisha ushindi wa kwanza wa Leverkusen tangu miaka 23 uwanjani Allianz Arena dhidi ya Bayern.

Michezo mingine jana ilizikutanisha Hannover 96 na Borussia Moenchengladbach. Hannover ilipoteza ushindi wa mabao 2-0 na kupigwa mwereka wa mabao 3-2 mwishoni katika mpambano huo, ambao ulikuwa wa vuta nikuvute.

HANNOVER, GERMANY - OCTOBER 28: Mario Eggimann (R) of Hannover and Igor de Camargo (L) of Gladbach battle for the ball during the Bundesliga match between Hannover 96 and Borussia Moenchengladbach at AWD Arena on October 28, 2012 in Hannover, Germany. (Photo by Martin Rose/Bongarts/Getty Images)
Hannover 96 - ikipambana na Borussia MönchengladbachPicha: Bongarts/Getty Images

Frankfurt nayo yagonga ukuta

Hapo kabla VFB Stuttgart iliizamisha Eintracht Frankfurt , ambayo imeanza msimu huu kwa kushangaza mashabiki wa soka kwa kushinda michezo yake sita ya mwanzo. Stuttgart hata hivyo haikuwa na kazi nyepesi kupata ushindi huo , lakini mabao 2-1 yalitosha kwa kikosi hicho cha kocha Bruno Labadia kurejea nyumbani na points tatu muhimu .

Borussia Dortmund ilipata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Freiburg katika mchezo ambao uamuzi pia ulilalamikiwa mno na Freiburg, kwamba mabao yote ya Dortmund hayakupaswa kukubaliwa, na Freiburg kunyimwa penalti, baada ya Leverndowski kuunawa mpira katika harakati za kuokoa langoni mwake.

VFL Wolfsburg ambayo imejitenga na kocha wake aliyeitawaza bingwa miaka minne iliyopita Felix Magath, wiki iliyopita , imefanya maajabu kwa ushindi wa mabao 4-1 nyumbani kwa Fortuna Dusseldorf siku ya Jumamosi na kuchupa kutoka mkiani mwa ligi na kushika nafasi ya tatu kwa kuwa na points nane.

DUESSELDORF, GERMANY - OCTOBER 27: Ivica Olic (2nd R) of Wolfsburg celebrates with his team mates after scoring his team's second goal during the Bundesliga match between Fortuna Duesseldorf 1895 and VfL Wolfsburg at Esprit-Arena on October 27, 2012 in Duesseldorf, Germany. (Photo by Joern Pollex/Bongarts/Getty Images)
Wachezaji wa VfL Wolfsburg wakishangiria bao dhidi ya DusseldorfPicha: Bongarts/Getty Images

Huko Uingereza jana Jumapili(28.10.2012) soka ya nchi hiyo iliingiwa na mdudu tena kutokana na madai ya ubaguzi na timu kubebwa na waamuzi. FC Chelsea imetoa madai rasmi kuhusiana na lugha, ambayo inaripotiwa kuwa , refa wa mchezo huo dhidi ya Manchester United aliitoa dhidi ya wachezaji wawili wa Chelsea jana, katika matokeo yenye utata , ambapo Chelsea ilicheezea kipigo cha mabao 3-2 dhidi ya Man United.

Manchester United players including Wayne Rooney, centre take part in one minute applause for Bolton Wanderers' Fabrice Muamba who suffered a cardiac arrest during his team's FA Cup match against Tottenham before their English Premier League soccer match against Wolverhampton Wanderers at Molineux Stadium, Wolverhampton, England, Sunday, March 18, 2012. (Foto:Jon Super/AP/dapd)
Kikosi cha Manchester UnitedPicha: AP

Kabla ya hapo mashabiki wa soka walishuhudia bao la ushindi la Liverpool likikataliwa na mwamuzi akidai mfungaji wa bao hilo Suarez alikuwa ameotea. Lakini bao la ushindi la Manchester United lilikubaliwa hata kama mfungaji wa bao hilo Chicharito alionekana kutokea katika nafasi ambayo alikuwa ameotea.

Moyes ataka kadi nyekundu

Wakati huo huo kocha wa Everton David Moyes anahisi kuwa Luis Suarez wa Liverpool alipaswa kutolewa nje kwa kadi nyekundu hata kabla ya juhudi za mwisho za mshambuliaji huyo wa Liverpool kupata bao la ushindi dakika za mwisho za mchezo huo kukataliwa na mwamuzi katika mchezo wao wa watani wa jadi wa Merseyside.

Kwa mara nyingine tena raia huyo wa Uruguay alikuwa kivutio katika uwanja wa Goodison Park, baada ya kupachika bao la kwanza ambalo liliingizwa wavuni na mchezaji wa Everton , Leighton Baines mapema katika mchezo huo na kisha Luis Suarez kushangiria kwa kujitupa chini miguuni mwa kocha wa Everton , Moyes.

Uruguay's Luis Suarez celebrates his third goal against Chile during a 2014 World Cup qualifying soccer game in Montevideo, Uruguay, Friday, Nov. 11, 2011. (Foto:Matilde Campodonico/AP/dapd)
Luis Suarez raia wa Uruguay ambaye ni mchezaji wa LiverpoolPicha: dapd

Kabla ya mchezo huo , kocha wa Everton alikuwa na mawazo kuwa Suarez hujiangusha kirahisi langoni mwa adui na kwamba kitendo kama hicho husababisha mashabiki kutokuja uwanjani kushuhudia pambano.

Cristiano atamba

Katika La Liga nchini Uhispania Gonzalo Higuain na Cristiano Ronaldo walipachika kila mmoja mabao 2 wakati wa ushindi wa Real wa mabao 5-0 dhidi ya Mallorca jana na kuendelea kuweka mbinyo katika timu zinazoongoza ligi hiyo.

Wakati huo huo Atletico Madrid iliishinda Osasuna kwa mabao 3-1 na kuendelea kuwa sawa na Barcelona kwa points.

epa03276008 Portuguese forward Cristiano Ronaldo celebrates at the final whistle of the quarter final match of the UEFA EURO 2012 between the Czech Republic and Portugal in Warsaw, Poland, 21 June 2012. EPA/MARIO CRUZ UEFA Terms and Conditions apply http://www.epa.eu/downloads/UEFA-EURO2012-TCS.pdf +++(c) dpa - Bildfunk+++
Cristiano RonaldoPicha: picture-alliance/dpa

Viongozi wa Serie A Juventus Turin imeendelea kupeta kwa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Catania baada ya timu hiyo kutoka kisiwa cha Sicily kupata bao ambalo lilionekana kuwa halali lakini mwamuzi alilikataa.

Bao la Juve hata hivyo lilionekana kuwa si halali kwa kuwa mshambuliaji Nicklas Bendtner alikuwa ameotea wakati alipopiga mpira ambao uliokolewa na mlinda mlango wa Catania na kusababisha Arturo Vidal kuukwamisha mpira huo wavuni.

Na huko nchini Argentina, lile pambano la watani wa jadi ambalo linazungumziwa kuwa huwa la aina ya pekee duniani kwa ushindani , lilimalizika kwa sare ya mabo 2-2 kati ya Boca Juniors na River Plate.

Tennis.

Victoria Azarenka kutoka Belarus hajashinda ubingwa wa chama cha Tennis duniani , WTA , lakini kufikia nusu fainali kumemhakikishia kushika nafasi ya kwanza katika orodha ya wachezaji bora wa tennis kwa upande wa wanawake msimu huu.

Victoria Azarenka of Belarus hits a backhand return to Maria Sharapova of Russia during the women's singles final at the Australian Open tennis championship in Melbourne, Australia, Saturday, Jan. 28, 2012. (Foto:Sarah Ivey/AP/dapd).
Mchezaji Victoria Azarenka wa BelarusPicha: AP

Azarenka anafuatiwa na Maria Sharapova wa Urusi pamoja na Serena Williams wa Marekani akishika nafasi ya tatu.

Kwa upande wa wanaume mchezaji anayeongoza orodha hiyo ni Roger Federer wa Uswisi, akifuatiwa na Novak Djokovic wa Serbia na Andy Murray wa Uingereza anashikilia nafasi ya tatu.

Mwandishi : Sekione Kitojo / afpe / dpae / rtre / zr

Mhariri : Mohammed Abdul-Rahman