1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BEIJING: Daraja laporomoka na kuuwa watu 36

17 Agosti 2007
https://p.dw.com/p/CBYd

Idadi ya watu waliopoteza maisha yao baada ya daraja kuporomoka,kusini mwa China,imefikia 36 na wengine 23 bado hawajulikani walipo.Daraja hilo katika wilaya ya Hunan,lilikuwa bado likijengwa. Maafisa wanasema,kuna matumaini madogo ya kukuta watu walionusurika,kwa sababu wakuu wa afya wameanza kunyunyuiza dawa katika maji,ili kuzuia uambukizaji wa magonjwa.