BEIJING :Indonesia na Uchina kuchimba mafuta Sudan
2 Julai 2007Matangazo
Makampuni ya serikali ya Uchina na Indonesia wametia saini makubaliano ya kuchimba mafuta nchini Sudan kwa mujibu wa gazeti moja la Uchina.Ripoti hiyo inatolewa huku jamii ya kimataifa ilikalumu Uchina kwa kuwekeza kwa kiwango kikubwa kwenye sekta ya mafuta nchini Sudan.Hatua hiyo inaaminika kuiwezesha Sudan kukataa shinikizo za mataifa ya kigeni katika suala la umwagikaji wa damu kwenye eneo la Darfur.
Mkataba huo wa miaka ishirini wa kuchimba mafuta unahusisha kampuni ya kitaifa ya mafuta ya Uchina na PT Pertamina ya Indonesia.