1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BEIRUT: Majadiliano ya kuunda serikali ya umoja yavunjika

12 Novemba 2006
https://p.dw.com/p/CCtW

Mgogoro wa kisiasa nchini Lebanon umezidi kuwa mkali.Waziri mkuu Fuad Siniora amekataa kukubali kujiuzulu kwa mawaziri watano wa Kishia. Inasemekana kwamba madai ya mawaziri hao kutaka makundi ya Hezbollah na Amal,yanayoiunga mkono Syria kuwa na usemi zaidi bungeni, hayakutimizwa.Stesheni ya televisheni ya Washia- Al Manar-imeripoti kuwa majadiliano yalioitishwa na Hezbollah,kuunda serikali ya umoja wa taifa yamevunjika.