1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BEIRUT: Wahezbollah wataka kubadilishana wafungwa

29 Julai 2007
https://p.dw.com/p/CBeB

Nchini Lebanon,kiongozi wa chama cha Hezbollah chenye sera kali amesema wanajeshi 2 wa Kiisraeli waliotekwa nyara mwaka mmoja uliopita wataachiliwa huru kwa kubadilishana wafungwa tu. Sheikh Hassan Nasrallah,alitamka hayo katika hotuba yake kwenye televisheni.Chama cha Hezbollah kiliwateka nyara wanajeshi hao wawili Julai mwaka jana,hatua iliyoifanya Israel kuanzisha vita vya mwezi mmoja dhidi ya Hezbollah.