Bekele ajiandaa kwa mbio za Paris marathon
4 Aprili 2014Matangazo
Mwanariadha huyo aliyeweka rekodi mbili za ulimwengu katika mbio za mita 5,000 na 10,000 ataangaziwa macho katika mbio hizo za Paris Marathon, kuona kama atafaulu kufanya vyema katika marathon. Anasema ana nafasi nzuri kwa sababu amefayna mazoezi ya kutosha na atakimbia ili kupata ushindi.
Baada ya kuwa na taaluma nzuri katika mbio za masafa mafupi, mwanariadha huyo mwenye umri wa miaka 31 anataraji kufuata nyayo za Mfalme wa Ethiopia Haile Gebreselassie, ambaye alifaulu kubadilisha taaluma yake kutoka mbio za uwanjani hadi zile za marathon.
Mwandishi: Bruce Amani/AFP/DPA
Mhariri: Mohammed Abdul-Rahman