1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BERLIN: Kesi mpya za homa ya mafua ya ndege

6 Julai 2007
https://p.dw.com/p/CBlY

Wataalamu nchini Ujerumani na Ufaransa wanaimarisha hatua za kinga dhidi ya homa ya mafua ya ndege.Hatua hizo zimechukuliwa baada ya maafisa wa Kijerumani kuripoti kesi 38 mpya katika jimbo la Saxony-Anhalt,ikihofiwa kuwa zinahusika na virusi vya H5N1.Tangu mwisho wa mwezi uliopita,Saxony-Anhalt ni jimbo la nne kutoka majimbo 16 ya Ujerumani kuripoti homa ya mafua ya ndege.