1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BERLIN : Merkel azungumza na Abbas na Olmert

14 Juni 2007
https://p.dw.com/p/CBrw

Kansela Angela Merkel wa Ujerumani amezungumzia ongezeko la wimbi la umwagaji damu wa Gaza na Rais Mahamoud Abbas wa Palestina halikadhalika Waziri Mkuu wa Israel Ehud Olmert.

Merkel amerudia tena kuunga mkono juhudi za kutafuta amani za Rais wa Palestina wakati wa mazungumzo yake hayo kwa njia ya simu.

Maafisa mjini Berlin wamesema Olmert pia ameelezea kuwa tayari kwake kuendelea kushirikiana na Abbas.