1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BERLIN :Waziri atetea kubinafsisha nusu ya shirika la reli

21 Septemba 2007
https://p.dw.com/p/CBNo

Waziri wa uchukuzi wa Ujerumani Wolfgang Tiefensee ametetea mipango yake kuuza asilimia 49 ya shirika la reli linalomilikiwa na taifa la Deutsche Bahn wakati wa mjadala katika bunge la Ujerumani.

Amesisitiza kwamba kubinafisha nusu ya shirika hilo kutaifanya kampuni hiyo kumudu zaidi ushindani wa kimataifa na ameahidi huduma za reli zitaboreshwa.

Mjadala huo unakuja siku moja baada ya kusambaratika kwa mazungumzo kati ya chama cha wafanyakazi madereva wa shirika hilo la GDL na waajiri.

Chama hicho cha wafanyakazi kimekuwa kikishinikiza ongezeko la mshahara la asilimia 31 ambapo Deutsche Bahn imeeleza kuwa ni dhihaka.