BRASILIA:Brazil yaomboleza vifo vya ajali ya ndege
1 Oktoba 2006Matangazo
Rais Lula da Silva wa Brazil ametangaza siku tatu za maombolezo kufuatia ajali ya ndege ambapo watu 155 wamekufa.
Habari zinasema hakuna alienusurika katika ajali ya ndege hiyo iliyoanguka katika misitu ya Amazon.
Askari waliopelekwa katika sehemu hiyo ya ajali walilazimika kufyeka misitu mikubwa ili kuziwezesha helikopta kutua.
Ndege hiyo ya abiria ilikuwa inatoka mji wa Manaus kaskazini mwa Brazil ikielekea mji mku Brasilia.
Kilichosababisha ajali ya ndege hiyo bado hakijajulikana lakini maafisa wa usafiri wa anga wanatuhumu kuwa iligongana na ndege nyingine ndogo iliyoweza kutua salama baada ya dafrao hiyo.