1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

CAIRO: Kansela wa Ujerumani Angela Merkel aanza ziara ya Mashariki ya Kati.

4 Februari 2007
https://p.dw.com/p/CCV7

Kansela wa Ujerumani, Bibi Angela Merkel, ameanza ziara yake ya siku nne Mashariki ya Kati kwa mashauriano na Rais wa Misri, Hosni Mubarak, mjini Cairo.

Viongozi hao wamesisitiza haja ya mkakati wa pamoja wa kimataifa kufufua mashauriano ya amani kati ya Israil na Wapalestina.

Bibi Angela Merkel ameipongeza Misri kwa jitihada zake ambazo hazijafanikiwa za kuvipatanisha vyama hasimu vya Wapalestina.

Kansela huyo wa Ujerumani anatarajiwa pia kuzitembelea Saudi Arabia, Muungano wa Mataifa ya Kiarabu, na Kuwait.