1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

CARACAS:Castro asikika kwenye kipindi cha mojakwa moja Redioni

28 Februari 2007
https://p.dw.com/p/CCO3

Rais wa Cuba Fidel Castro amesema anaendelea kupata nafuu na kujisikia mwenye nguvu baada ya kuugua maradhi ya tumbo.

Castro aliyasema hayo akizungumza moja kwa moja katika kipindi cha redio pamoja na mshirika wake rais wa Venezuela Hugo Chavez.

Tukio hilo limewashtukiza wasikilizaji ambao hawakutarajia kumsikia kwa sasa kiongozi huyo kutokana na hali yake ya kiafya.