1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Champions League yaanza leo

18 Februari 2014

Mashindano ya kombe la vilabu bingwa barani Ulaya -Champions League yanaanza leo tarehe 18.02.2014 huku klabu ya Bayer Leverkusen ya Ujerumani ikichuana na Paris St Germain (PSG) ya Ufaransa.

https://p.dw.com/p/1BB29
Champions League mchuano kati ya FC Bayern Munich na Manchester City mwaka 2013
Champions League mchuano kati ya FC Bayern Munich na Manchester City mwaka 2013Picha: picture-alliance/dpa

Manchester City ya Uingereza nayo inaikaribisha Barcelona ya Uhispania. Kesho tarehe 19.02.2014 Mabingwa wa Ujerumani na ulaya Bayern Munich watakuwa mjini London kwa pambano dhidi ya Arsenal ya Uingereza. Hadi sasa Bayern haikupoteza hata mchezo mmoja katika ligi kuu ya nyumbani Bundesliga, ikiwa na pointi 16 zaidi ya Bayer Leverkusen inayoshika nafasi ya pili.

Mhariri: Mohamed Abdulrahman