1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Sayansi

Wanasayansi wawili washinda tuzo ya Nobeli ya tiba

Amina Mjahid
2 Oktoba 2023

Wanasayansi wawili Katalin Kariko na Drew Weissman wameshinda tuzo ya Nobeli ya masuala ya tiba kwa juhudi zao za kutengeneza chanjo za COVID 19 kwa kutumia teknolojia mambo leo ya mRNA.

https://p.dw.com/p/4X3LG
Watafiti wa kisanyansi walioshinda Tuzo ya Amani ya Nobeli katika masuala ya tiba Katalin Kaliko(kushoto) na Drew Weissman(kulia)
Watafiti wa kisanyansi walioshinda Tuzo ya Amani ya Nobeli katika masuala ya tiba Katalin Kaliko(kushoto) na Drew Weissman(kulia)Picha: EUGENE HOSHIKO/AFP

Jopo la majaji wa tuzo hiyo limesema wawili hao wamechangia kutengenezwa kwa kasi chanjo hiyo wakati dunia ilipokabiliwa na kiticho kikubwa kwa afya ya binaadamu.

Chanjo za mRNA ziliidhinishwa kutumika mwezi Desemba mwaka 2020 na pamoja na chanjo nyengine ya Covid zikasaidia kuokoa maisha ya mamilioni ya watu na kuzuwiya magonjwa makali kwa watu wengi zaidi.

Kariko, aliye na miaka 68, na  Weissman, aliye na miaka 64, waliofanya kazi kwa muda mrefu pamoja katika chuo cha Pennsylvania, Marekani wameshinda tuzo nyengine kadhaa ikiwemo tuzo ya Lasker mwaka 2021.