1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Chavez azuru Iran

18 Novemba 2007
https://p.dw.com/p/CIlz

TEHERAN:

Rais Hugo Chavez wa Venezuela anatazamiwa kuwasili jioni ya leo mjini Teheran,kutoka Saudi Arabia, hivyo akibainisha tena usuhuba mkubwa kati ya mahasimu hawa 2 wa Marekni.

Rais Chavez ataandamana na mawaziri 5 miongoni mwao waziri wake wa mambo ya nje,m yule wa mafuta na waviwanda.

Msemaji wa wizara ya nje ya Iran Mohammed Ali Hosseini amesema rais huyo wa Venezuela atatia saini mapatano juu ya ushirikiano wa kiviwanda wakati wa ziara yake hiyo ya siku 1.lHii itakua ziara ya 4 ya rais Chave nchini Iran tangu rais Ahmadinejad kushika madaraka 2005.Ziara yake ya mwisho mjini Teheran ilikua July, mwaka huu alipojenga msingi pamoja na rais Ahmadinejad wa kiwanda cha pamoja cha petroli.Ziara ya mwisho ya rais wa Iran nchini venezela, ilikua Septemba.Ilikua ni ya 3.