1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

C.Ndereba bingwa wa Marathon Osaka

2 Septemba 2007
https://p.dw.com/p/CBTW

RIADHA:OSAKA:

Catherine Ndereba amenyakua medali ya 4 ya dhahabu kwa Kenya mapema leo asubuhi kutoka mbio za Marathon.Ndereba alishinda taji hili tayari katika mashindano kama haya ya ubingwa wa dunia 2003 na akabidi kuridhika na medali ya fedha mwaka 2005.Muda wake ulikuwa masaa 2:30 na sek.37.Mchina Zhou Chunxiu alikuja wapili huku mwenyeji mjapani Reiko Tosa alitwaa medali ya shaba.

Tayari jana,muethiopia Meserat Dibaba ,alitamba katika mbio za mita 5000 ambamo ni bingwa pia wa olimpik na rekodi ya dunia.