1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

COLOGNE:Ujerumani yaomboleza vifo vya askari wake

24 Mei 2007
https://p.dw.com/p/CByz

Ujerumani inaomboleza vifo vya askari wake watatu waliyouawa Jumamosi iliyopita huko Afghanistan.

Miili ya wanajeshi hao iliwasili jana mjini Cologne katika uwanja wa ndege wa jeshi, na katika misa ya wakfu baadaye, waziri wa ulinzi wa Ujerumani, Franz Josef Jung alisema kuwa wanajeshi hao walikuwa katika kikosi cha ujenzi huko Kunduz.

Amesema kuwa Ujerumani itaisaidia serikali ya Afghanistan kuwapata wauaji wa wanajeshi hao na kuwafikisha mbele ya sheria.

Wakati huo huo Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani, Frank-Walter Steinmeir, amezitaka Pakistan na Afghanistan kuongeza ushirikiano ambao utasaidia kuwasambaratisha wataliban

Waziri Steinmeir alisema hayo mjini Islamabad baada ya mazungumzo yake na waziri mwenziye wa Pakistan.

Pakistan imekuwa iklaumiwa ya kwamba imeshindwa kudhibiti mpaka wake, ambao unatumiwa na wapiganaji wa Taliban kuingia Afghanistan kufanya hujuma