1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

COLOMBO: Boti za Tamil Tigers zimezamishwa

29 Machi 2007
https://p.dw.com/p/CCEV

Kwa mujibu wa jeshi la Sri Lanka,wanamaji wamezamisha boti tatu za waasi wa Tamil Tigers nje ya pwani,kaskazini-mashariki ya nchi na si chini ya waasi 15 wameuawa.Shambulio hilo ni mlolongo wa mashambulio ya hivi karibuni katika ardhi kavu na baharini kati ya waasi na vikosi vya serikali nchini Sri Lanka.Vita vya wenyewe kwa wenyewe vya miongo miwili,vimeua kiasi ya watu 68,000 nchini humo.Pande zote mbili sasa zimepuuza makubaliano ya kuweka chini silaha yaliotiwa saini mwaka 2002.