1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Deutsche Bank yapata viongozi wapya

31 Mei 2012

Benki ya Ujerumani-Deutsche Bank inapata uongozi mpya kuanzia kesho,kufuatia kumalizika kwa enzi ya mwenyekiti maaruf wa benki hiyo Josef Ackermann

https://p.dw.com/p/155DE
Viongozi wapya wa Deutsche Bank Anshu Jain na Jürgen Fitschen
Viongozi wapya wa Deutsche Bank Anshu Jain na Jürgen FitschenPicha: picture-alliance/dpa

Kuanzia hapo kesho benki  hiyo kubwa kabisa nchini Ujerumani itaongozwa na watu wawili Anshu Jain na Jürgen Fitschen.

.Wenye hisa zaidi ya alfu tano katika  Benki hiyo ya Ujerumani  wanatarajiwa kuhudhuria mkutano wa mwaka wa Benki hiyo ambapo wenyeviti wenza watakaoiongoza watatambulishwa mjini Frankfurt. Pamoja na Mjerumani Jürgen  Fitschen ni Anshu Jain kutoka India.

Siyo lazima kiongozi wa benki hiyo awe Mjerumani  na hivyo moja kwa moja kuweza kuwa mshirika muhimu wa mazungumzo na serikali ya  Ujerumani. Dhima hiyo ilitimizwa na viongozi waliotangulia Hermann-Josef Abs,Alfred Herrhausen na Josef Ackermann ambaye ni Mswisi. Kansela wa Ujerumani Angela Merkel hata alifikia hatua  ya kuandaa tafrija kwa heshima ya bwana Ackermann aliekuwa anatimiza umri wa miaka 60 japo hafla hiyo haikupita bila ya utata.

Lakini Bwana Ackermann anaagwa baada ya kuiongoza Deutsche Bank kwa muda wa miaka kumi. Jee wanaomfuatia wanazo sifa kama zake?

Christoph Schalast kutoka chuo cha usimamizi wa fedha cha mjini Frankurt amesema kuwa kwanza inapasa mtu afanye kazi ili kuzifikia sifa hizo, inapasa kufanya afanye  kazi ili kujenga imani na mtu mkimya kwa kiasi cha kutosha.Bwana Schalast ameeleza kuwa haipasi kwa mtu kuwa mbinafsi mwenye  tabia ya kujinufaisha yeye mwenyewe,  anatakiwa awe na uwazi na awe mshauri wa dhati . Amesema watakaomfuatia watakuwa na changamoto ya kuonyesha kwamba wanayaweza hayo.

Watakaomfuatia, Jürgen  Fitschen na Anshu Jain watakuwa na jukumu la kuwasaidia wenye hisa katika  kupata faida ya hisa  zao. Wakati wa  uongozi wa Ackermann thamani ya hisa  zilipanda na  kushuka. Mwanzoni kabisa wakati  Ackermann alipokuwa msemaji wa bodi ya uongozi hisa zilikuwa na thamani ya  Euro 76.

Mnamo mwaka wa 2007 zilivuka thamani ya Euro 118 lakini hadi  kufikia mwezi januari mwaka 2009 thamani ilishuka hadi Euro 15 tu. Kwa jumla, katika kipindi cha miaka 10 iliyopita thamani ya hisa za Deutsche Bank imeanguka kwa asilimia 60.Kwa hiyo ilikuwa vizuri kwa wateja  walioziweka  fedha zao katika vitabu vya akiba ya benki kwa njia ya kawaida.

Ili kuibadilisha hali hiyo itapasa katika siku za neema kuwekeza katika shuhguli za kuzalisha mitaji. Lakini katika hilo Deutsche Bank ilikabiliwa na tajiriba mbaya wakati wa mgogoro wa mabenki ulioikumba  dunia.. Badala ya kuwa mdhamini wa mashaka ikawa mfanya biashara  za mashaka na ilipeleka dhamana nyingi  za mashaka kwenye soko.

Viongozi wapya watakuwa na  changamoto ya kutafuta wizani baina ya ugeugeu katika vitega  uchumi katika uzalishaji wa mitaji na biashara imara na makampuni na  wateja binafsi. Chini ya uongozi wa Ackermann kulikuwa na mpango wa kuzalisha nusu ya mapato kutokana na  kuwekeza katika shughuli za kuzalisha mitaji -investment banking.

Mwandishi:Braun,Michael

Tafsiri;Mtullya Abdu

Mhariri:Hamidou Oummilkheir