1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Dortmund yapanda hadi nafasi ya pili

29 Novemba 2012

Ligi ya Ujerumani Bundesliga yakamilisha mchezo wake wa 13,Bayern Munich yaiadhibu Hannover 96mabao 5-0, hata hivyo ligi hiyo inarejea tena uwanjani kesho Jumanne(27.11.2012)kunaanza mchezo wa14.

https://p.dw.com/p/16q8S
Nach Spielende bedanken sich die Spieler des BVB bei den Fans Fussball 1.Bundesliga: 1.FSV Mainz 05 - BVB Borussia Dortmund, Mainz, 24.11.2012 -- Football, Soccer 1st. Division: 1.FSV Mainz 05 vs. BVB Borussia Dortmund, Mainz, November 24, 2012
BVB Borussia Dortmund baada ya ushindi dhidi ya MainzPicha: picture alliance/GES-Sportfoto

Bayer Leverkusen  imepata  ushindi  wa  mabao  2-1  dhidi  ya  TSG Hoffenheim   na  kujiimarisha  katika  nafasi  ya  tano  ya  msimamo wa  ligi. Kwa  ushindi  wa  jana  wa  kikosi  cha  kocha  Sascha Lewandowski unakuwa  ushindi  wa  saba  katika  msimu  huu.

FC Augsburg  na  Borussia  Moenchengladbach  hazikuonyesha wa kusisimua  sana  jana  na  waliridhika  na  sare  ya  bao 1-1.

Ushindi  mnono  ulikwenda  kwa  SC  Freiburg, ambapo  iliizaba  VFB Stuttgart  kwa  mabao  3-0  na  Freiburg  ikachupa  hadi  nafasi  ya sita  katika  msimamo  wa  ligi.

Dortmund yakwea juu

Borussia  Dortmund , ambao  ndio  mabingwa  watetezi  wa  ligi  hiyo wametoka  nafasi  ya  nne  na  kuchipa  hadi  nafasi  ya  pili, ikiwa sasa  inaiwinda  Bayern  Munich, ambayo  siku  ya  Jumamosi ilifanya  mauaji  makubwa  dhidi  ya Hannover  96  kwa  kuichapa mabao 5-0 nyumbani.

Bayern Munich's Dante (L-R), Philipp Lahm, Javi Martinez, Toni Kroos and Franck Ribery celebrate their victory after their German first division Bundesliga soccer match against Hanover 96 in Munich November 24, 2012. Bayern Munich won the match 5-0. REUTERS/Michaela Rehle (GERMANY - Tags: SPORT SOCCER) DFL RULES TO LIMIT THE ONLINE USAGE DURING MATCH TIME TO 15 PICTURES PER GAME. IMAGE SEQUENCES TO SIMULATE VIDEO IS NOT ALLOWED AT ANY TIME. FOR FURTHER QUERIES PLEASE CONTACT DFL DIRECTLY AT + 49 69 650050
Bayern Munich wakisherehekea karamu ya magoli dhidi ya HannoverPicha: Reuters

Dortmund  ilihitaji  kufanyakazi  ya  ziada  kupata  ushindi  wa  mabao 2-1  dhidi  ya  majirani  zao  wa  Mainz 05.

Baden-Wuerttemberg/ Fussball, 1. Bundesliga, Saison 2012/13, 13. Spieltag, SC Freiburg - VfB Stuttgart, Sonntag (25.11.12), Mage-Solar-Stadion, Freiburg: Freiburgs Trainer Christian Streich. (zu dapd-Text) +++ Achtung Bildredaktionen: Die Verwendung der Bilder fuer die gedruckten Ausgaben der Zeitungen und andere Print-Medien ist ohne Einschraenkungen moeglich. Die DFL erlaubt ausserdem die Publikation und Weiterverwertung von maximal 15 Fotos (keine Sequenzbilder und keine videoaehnlichen Fotostrecken) aus dem Stadion und/oder vom Spiel im Internet und in Online-Medien. Die Publikation oder Verwertung der Fotos (Stand- und Sequenzbilder) aus dem Stadion und/oder vom Spiel ueber Mobilfunk (insbesondere per MMS) und ueber DVB-H/SH und DMB ist erst 2 Stunden nach Abpfiff des jeweiligen Spiels erlaubt!
Kocha wa SC Freiburg - Christian StreichPicha: dapd

Pambano  lililokuwa  likisubiriwa  kwa  hamu  hata  hivyo  ni  kati  ya VFL  Wolfsburg  ambayo  ikiwa  na  meneja  mpya  Klaus Allofs ilikuwa  inapambana  na  Werder  Bremen  ambayo  ni  wiki  iliyopita tu  meneja  huyo  alikuwa  akiitumikia. Mpambano  huo  uliongezwa hamasa  na  kuhama  kwa  Klaus Allofs  kutoka  Werder Bremen  na kwenda  VFL Wolfsburg. Hata  hivyo  pambano  hilo  lilimalizika  kwa sare  ya  bao 1-1.

Real yateleza

Huko  nchini  Hispania, mabingwa  watetezi Real Madrid  waliteleza pale  walipokubali  kipigo  cha  bao  1-0  dhidi  ya  Real Betis, ikiwa ni  kipigo  cha  tatu  katika  kampeni  ya  msimu  huu  kwa  kikosi  cha kocha  Jose Mourinho.

Viongozi  wa  ligi  hiyo  Barcelona  pamoja  na  timu  iliyo  katika nafasi  ya  pili Atletico Madrid  wamefanikiwa  kuweka  kasi  yao  ya kusonga  mbele  jana, wakati  Barca  ilipoibamiza  Levante  kwa mabao 4-0  na  Altelico  ikainyuka  Sevilla  kwa  kiwango  kama hicho  cha  mabao 4-0.

Katika  Premier League  Manchester United  ilifanikiwa  kurejea kileleni  mwa  msimamo  wa  ligi  baada  ya  ushindi  wa  mabao 3-1 dhidi  ya  Queens Park Rangers, wakati  mabingwa  Manchester City  wakiridhika  na  sare  ya  bila  kufungana  na  Chelsea  . Kocha  Rafa Benitez  alikuwa  akisimamia  mchezo  wake  wa kwanza   baada  ya  kurejea  katika  Premier League. Mapokezi  ya Benitez  kwa  mashabiki  wa  Chelsea  hayakuwa  mazuri, wengine wakipaaza  sauti  kuwa  hatakiwi  katika  klabu  hiyo  na  wengine wakitabiri  kuanguka  kwake  kwa  haraka. Mashabiki  walikuwa katika  mchezo  huo  wakimwagia  sifa  na  kuimba  jina  la  kocha wa  zamani  aliyetimuliwa  Roberto Di Matteo.

Chelsea's interim head coach Roberto Di Matteo blows his whistle during a Champions League final training session at the club's training ground in Stoke D'Abernon, England, Tuesday, May 15, 2012. Chelsea are due to play Bayern Munich in the final of the Champions League in Germany on Saturday. (Foto:Matt Dunham/AP/dapd).
Kocha wa zamani wea Chelsea Roberto Di Matteo, anayependwa na mashabikiPicha: dapd

Lakini Benitez  anadai kuwa  hana  wasi  wasi  kwa  kuwa  ushindi  utawafanya  mashabiki hao  kusafiri  nae  katika  ngalawa  moja.

Huko  Italia  viongozi  wa  ligi  ya  Italia, Serie A  ambao  pia  ndio mabingwa  watetezi Juventus Turin  wameangukia  pua  jana  kwa kipigo cha  bao  1-0  dhidi  ya  AC Milan kwa  bao  la  penalti  la Robinho.

Juve  inaongoza  kwa  kuwa  na  points 32  kutoka michezo  14  huku  Inter Milan  ikiwa  nyuma  kwa  points  nne  kabla ya  pambano  lao  hii  leo  Jumatatu  dhidi  ya  Parma. Fiorentina iliyo  katika  nafasi  ya  tatu  ilitosheka  na  sare  ya  mabao 2-2 dhidi  ya  Torino jana  Jumapili.

Paris St Germain  inaongoza  ligi  ya  Ufaransa  ikifuatiwa  na Olympique Marseille  kwa  tofauti  ya  magoli, na  timu  hiyo  ina miadi  na  Olympique Lyon  siku  ya  Jumatano.

Bundesliga  yarejea  tena  uwanjani

Ligi  ya  Ujerumani  Bundesliga  inarejea  uwanjani  kesho jioni ambapo  timu   zitaingia  uwanjani  katika  mchezo  wa  14  wa  ligi hiyo. Mabingwa  watetezi  Borussia  Dortmund  itakuwa  na  kibarua na  Fortuna  Düsseldorf, Frankfurt  itakuwa  nyumbani  ikiwakaribisha Mainz 05, Hannover  iliyojeruhiwa  siku  ya  Jumamosi  itatafuta  njia ya kulipiza  kisasi  dhidi  ya  Greuther Fürth  na  Hamburg SV  ina miadi  na  Schalke 04.

Jumatano  itakuwa  zamu  ya  Stuttgart  ikikwaana  na  FC Augsburg, Werder  Bremen ikitiana  kifuani  na  Bayer Leverkusen , Borussia Moenchengladbach  inakwaana  na  VFL Wolfsburg  , Freiburg inawakaribisha  viongozi  wa  ligi  hiyo  Bayern Munich  nyumbani, wakati Nurnberg  itaonyeshana  kazi  na  Hoffenheim.

Na mashindano  ya  kuwania  ubingwa  wa  mataifa  ya  Afrika mashariki  na  kati  yameanza  rasmi  huko mjini  Kampala  Uganda, ambapo  timu  za  mataifa  12  ya  Afrika  mashariki  na  kati zinapambana. Wenyeji  wa  mashindano  hayo Uganda imeanza vizuri  kwa  ushindi  wa  bao 1-0  dhidi  ya  Kenya, na  Kilimanjaro Stars  ya  Tanzania  imeibwaga Sudan  kwa  mabao 2-0  jana Jumapili(25.11.2012), wakati  Burundi  ilipitisha  mipira  mara  tano   katika  nyavu za  Somalia . Somalia  iliambulia  bao moja. Katika pambano  kati  ya  Zanzibar  na  Eritrea,  matokeo  ni  sare  ya  bila  kufungana.   Mchezo  wa  pili  ni  kati  ya  Rwanda na  Malawi.

Mascot

Kila  mashindano  ya  fainali  za  kombe  la  dunia  kunakuwa  na kinyago cha  kuleta  bahati, maarufu  kama  mascot. Katika  fainali za  kombe  la  dunia  mwaka  2014  nchini  Brazil kinyago  hicho kimepewa  jina  la  Fuleco, zoezi  lililofanywa  kwa  ushirikiano  wa mashabiki  wa  soka  nchini  humo , limesema  shirikisho  la kandanda  duniani  FIFA  leo.

FIFA imesema  kuwa  asilimia  48  ya Wabrazil  waliohusika  katika  kura  hiyo  wamechagua  jina  la Fuleco  kuwa  jina  hilo, wakati   Zuzeco  limepata  asilimia  31 na Amijubi limepata  asilimia  21.

Fuleco  ni  mchanganyiko  wa maneneo Futebol, yaani  kandanda  na  ecologia  yaani  mazingira na  FIFA  imesema  uchaguzi  huo  unaonyesha  kuwa  Wabrazil wanajali  mazingira  kama  wanavyojali  kuhusu  soka. Kinyago  hicho kinatokana  na  umbo  la  mnyama  mwenye  asili  ya  Brazil anayejulikana  kama  Armadilo , na  kilichotakiwa  ni  armadilo kupata  jina.

Wakati  huo  huo  Wajerumani  wamesherehekea   ushindi  wa  dereva  bora  katika  mbio  maarufu  za  magari  za Formula 1, ambapo  Sebastian Vettel  alipata  ushindi  wake  wa  tatu katika  historia  ya  mbio  hizo. Dereva  huyo  wa  kundi  la  Red Bull alimaliza  akiwa  wa  sita  katika  mbio  hizo  zilizofanyika  nchini Brazil.

German Formula One driver Sebastian Vettel of Red Bull celebrates his third world championship in a row after the Formula One Grand Prix of Brazil at Autodromo Jose Carlos Pace in Sao Paulo, Brazil, 25 November 2012. Photo: David Ebener/dpa
Bingwa wa mbio za Formel 1 Sebastian Vettel wa UjerumaniPicha: picture-alliance/dpa

Lakini  kundi  la  magari  ya  Ferrari  limesisitiza  kuwa Vernando Alonso , ambaye  ameshika  nafasi  ya  pili , alipaswa kuwa  mtu  anayesherehekea  ushindi  wa  tatu, wakielekeza  kidole kwa  mbio  zenye  utata  zilizofanyika  nchini  Ubelgiji  na  Japan katika  kuelezea  hisia  zao.

Kwa  taarifa  hiyo  ya  mbio  za  magari  ndio sina  budi  kusema tumefikia  mwisho  wa  kuwaletea  habari  hizi  za  michezo  kwa  leo. Jina  langu  ni  Sekione  Kitojo, hadi  mara  nyingine  kwaherini.

Mwandishi : Sekione  Kitojo / rtre / afpe / dpae

Mhariri: Mohammed Abdul-Rahman