1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Dr. Koffi Annan atetea ripoti ya uchunguzi wa ghasia za uchaguzi nchini Kenya

19 Septemba 2008

Nchini Kenya katibu mkuu wa Umoja wa mataifa wa zamani Dr. Koffi Annan ametetea ripoti ya uchunguzi wa ghasia za uchaguzi uliofanyika nchini humo mwishoni mwa mwezi Disemba iliyopita.

https://p.dw.com/p/FLTi
Dr. Koffi AnnanPicha: AP

Dr. Annan ametoa wito kwa mapendekezo ya ripoti hiyo kutimizwa kwa minajili ya kuepuka ghasia za uchaguzi katika siku za usoni .Tume ya uchunguzi wa utata huo uliotokea mwaka uliopita iliongozwa na Jaji mstaafu wa Afrika Kusini Johann Christiaan Kriegler.Ghasia zilizuka baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2007 kufuatia utata ulitafutiwa ufumbuzi na Dr.Koffi Annan na kuwaleta pamoja mahasimu wa kisiasa walioafikiana kuunda serikali ya mseto.

Mwandishi wetu wa Nairobi Alfred Kiti alihudhuria mkutano wa Dr.Koffi Annan na kuandaa taarifa ifuatayo.