1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

EL-FASHER : Waasi wa Dafur wasusia mazungumzo

27 Oktoba 2007
https://p.dw.com/p/C7CU

Makundi mawili makuu ya waasi wa Dafur yamesema yatasusia mazungumzo ya amani yaliopangwa kuanza leo hii katika mji mkuu wa Libya Tripoli.

Kwa mujibu wa habari kutoka El-Fasher nchini Sudan hatua hiyo ni pigo kubwa kwa mazungumzo hayo ambayo Umoja wa Mataifa ilikuwa ikitumai kwamba yatapelekea kufikiwa makubaliano ya kudumu kwa jimbo hilo la Dafur lililoathiriwa na vita magharibi mwa Sudan.

Makundi hayo yanayosusia mazungumzo hayo ya amani ni ya Vuguvugu la Haki na Usawa na SLA-Unity ambalo linatuhumiwa kuhusika na mauaji ya wanajeshi 10 wa kulinda amani wa Umoja wa Afrika huko Dafur mwezi uliopita.