1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Eneo la Maghreb lavamiwa na Al Qaeda

Thelma Mwadzaya3 Februari 2010

Wakati Viongozi wa kundi la Al-Qaeda na Taliban wanapozungumza, kila mmoja huwa anaiangalia hali huko Pakistan, Iraq na Yemen.Al-Qaeda wako pia katika eneo la Afrika kaskazini

https://p.dw.com/p/LrAP
Kiongozi wa Al Qaeda Osama bin Laden na Ayman el Zawahiri.Picha: PA/dpa

Tawi  la   kigaidi  la  Waislamu  wenye  imani  kali linawateka  nyara  watu  kutoka  mataifa  ya  nje, linafanya biashara  ya  silaha  pamoja  na  madawa  ya  kulevywa  na kuna  kitisho  cha  kusambaa   vita  ya   jihad  hadi  katika nchi   yenye   matatizo  ya   kivita  ya  Nigeria.  Ripoti

Katika  eneo  la  jangwa  ambalo  halina   kitu  chochote  na mpaka  usiokuwa  na  mwisho  kati  ya  Algeria , Mauritania, Mali  na  Niger  kuna  eneo  tu  kama  linavyojulikana  kuwa halina  mwenyewe. Magaidi  na   waporaji   katika  eneo hilo  wanahifadhi  kila  kitu, silaha, madawa  ya  kulevywa, husafirisha   wahamiaji  haramu, wale  ambao  wanataka kuingia   katika  bara  la  Ulaya.  Na  katika  eneo  hili ambalo  haliingiliki, magaidi  wamefanikiwa  kulifanya  eneo lao  la  kujificha. Magaidi  wameweza  mara  kwa  mara kugonga  vichwa  vya  habari  kutokana  na  matukio  ya utekaji  nyara. Majira  ya  joto  ya  mwaka  2009  waliweza kumuua  mateka  wao   raia  wa  Uingereza.  Hii  ikiwa  ni alama  ya   kundi  la  al-Qaeda  kutoka  eneo  la  Afrika  ya kaskazini, ama  maghreb  kama  anavyoeleza  mtaalamu wa  masuala  ya  ugaidi  Mathieu  Guidere''Mateka kutoka  nchi  za  nje  kwa   magaidi  ni  kama  wafungwa wa  kivita,  ambao  hutumika  pia  kama  karata  turufu ya   kufanya  majadiliano, ili  kupata  fedha  ama kuweza  kuwatesa  wafungwa  wao. Ni  pale  tu   taifa  la Ulaya  magharibi  kama  katika   tukio  hili  la kusikitisha,  Uingereza , ilikataa  kufanya  majadiliano, ndipo  Al-Qaeda   huwauwa  mateka  wao.''

Mwakilishi wa Osama

Kundi  la  kigaidi  la  Al-Qaeda  liliundwa   mwishoni  mwa mwaka  2006  kutoka  katika  kile  kinachojulikana  kama GSPC, ambao  ni  mtandao  usiojulikana   wa   kigaidi nchini  Algeria.  Kiongozi  wake   wakati  huo  al-Zawahiri binafsi  alijitangaza  kuwa  mwakilishi  wa  Osama  bin Laden.  tangu  wakati  huo  kundi  hilo  la  eneo  la Maghreb  likapata  jina  la  al-Qaeda  katika  eneo  la maghreb  na  linaendesha  mambo  yake  lenyewe.  Kundi hilo  linahisi  kuwa   linalazimika  kufuata   nadharia  ya  al-Qaeda  nchini  Afghanistan,  licha  ya    kijifanyia    mambo yake  yenyewe. Mathieu  Guidere  anasisitiza   kuwa  al-Qaeda  katika  eneo  la  maghareb   haliangalii  tena mustakabali  wake  kuelekea  mataifa  ya  magharibi  nchini Algeria, bali  linataka  kupanua  shughuli  zake  katika sehemu  kubwa  zaidi  kuelekea  upande  wa  kusini, na kupeleka  kile  kinachojulikana   kama  vita   takatifu  katika eneo  lote la  jangwa  la  Sahara,  pamoja  na  Afrika kusini  mwa  jangwa  la  Sahara.''Mashambulio  ya kigaidi  pamoja  na  mateka   wengi  wanaokamatwa inamaana  ya   maafa  makubwa  kwa  utalii   katika eneo  hilo. Hofu   ya  mambo  hayo   inasababisha watu  wanaotaka  kusafiri  kwenda  katika  eneo  hilo kutoka  duniani  kote  kutofanya  hivyo  na  kuharibu uchumi  wa  mataifa  yanayohusika  kwa  kiasi kikubwa. Al-Qaeda    inaiona  biashara  ya  utalii  kama aina  mpya  ya  ukoloni   na  ubeberu, na  kwamba magaidi  hao   hawataki   kabisa   kuwaona  watu ambao  si  Waislamu  katika  maeneo  yao .''

Makundi haram

Athari  ya  kutengwa  na   mataifa  ya  magharibi  pia inaonekana  wazi  katika  maeneo  ya  kaskazini  ya  Nigeria ambako  kuna  masikini  wengi. Makundi  ya  kidini  kama Boko  Haram  yanajifananisha  na  Taliban   na  yanapigana ili  kuunda  taifa  la  Kiislamu,  na  kutokana  na   hali  hiyo baina  ya  Waislamu  wa  upande  wa  kaskazini  na Wakristo  wa  upande  wa  kusini  kila  mara  kuna  kuwa na  hali  ya  machafuko  na  watu  kwa  mamia  huuwawa. AQMI,  tawi  la  mtandao  wa  kigaidi  wa  al-Qaeda  upande wa   Afrika  kaskazini , linatumia  hali  hii  ya  wasi  wasi. Tayari  magaidi  wamekwisha  sema , nadharia  yao  ya Uislamu  wenye  msimamo   mkali   inayopata  nguvu nchini  Nigeria  ni  lazima  iendelezwe.  Kwa  kupeleka silaha   na  risasi  pamoja  na   mapambano. Mtaalamu  wa masuala  ya  ugaidi , Mathieu Guidere  anasema  kuwa  hilo lilikuwa  ni  suala  la  muda  tu, licha  ya  kuwa  , bado Nigeria  si  kituo  cha  al-Qaeda .  Lakini   hali  ni  tete. Katika  hali  hiyo  ya  wasi  wasi  kuna suala  la  serikali isiyo  na  kiongozi  ambapo  rais  anaendelea  kupata matibabu  nje  ya  nchi  hadi  leo .  Bila  shaka   Waislamu wenye  imani  kali  wanaendelea  kupata  wafuasi.

Katika  hali  hiyo  hicho  si  kitisho  kwa  eneo  la  jangwa  la Sahara  pekee.  Kundi  la  al-Qaeda  katika  eneo  la maghreb  hawakujiweka  tu  kufanya  ugaidi  katika   eneo la  jangwa,  lakini  pia  linalenga  maeneo  ya   mataifa magharibi. Kijana   wa  Ki-Nigeria Umar  Faruk Abdulmutallab, ambaye  alijaribu  kuilipua  ndege  mjini Detroit  ni  mmoja  kati  ya  watu  waliopata  mafunzo kutoka  kwa  al-Qaeda. Kama  tunaweza  kuyaamini mashirika  ya  kijasusi,  al-Qaeda  tayari   katika  eneo  la Maghreb  lina   vikundi   dazeni  vya  kigaidi  katika  mataifa ya  Ulaya. Kwa  sasa  wanasubiri  tu.

Mwandishi: Sekione  Kitojo / ZR

Mhariri: Thelma Mwadzaya.