1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Fabregas ainusuru Chelsea

16 Mei 2017

Mchezaji wa akiba Cesc Fabregas alifunga goli katika dakika ya 88 wakati mabingwa wapya wa ligi kuu ya England, Chelsea, walipowalaza Watford 4-3 usiku wa Jumatatu.

https://p.dw.com/p/2d2lZ
England Chelsea Meister Jubel
Kiungo wa Chelsea Cesc FabregasPicha: Reuters/Sibley Livepic

Mechi hiyo ya ligi iliyochezwa katika uga wa Stamford Bridge ilikuwa na mbwembwe chungu nzima.

Nahodha wa the blues John Terry alicheza mechi yake ya 716 na akatia kimyani bao la kwanza ila alifanya makosa na kumpelekea Etienne Capoue kusawazisha. Cesar Azpilicueta na Mitchy Batshuayi walifunga baadaen na kuwaweka Chelsea juu 3-1, lakini Stefano Okaka alifunga goli la kusawazisha baada ya Daryl Janmaat kuwafungia Watford la pili.

Lakini Cesc Fabregas alipachika wavuni goli la nne na kuwapa mabingwa hao wapya ushindi na kuwaweka katika nafasi ya kuwa timu ya kwanza kushinda mechi 30 katika ligi hiyo yenye mechi 38 kwa kila timu, lakini hilo litafanyika iwapo watashinda mechi yao ya mwisho mnamo wikendi, kwani kwa sasa wameshinda mechi 29.

"Kuna uwezekano wa kushinda mechi 30 na ni lazima tujaribu kulifikia lengo hilo sasa," alisema kocha wa Chelsea Antonia Conte baada ya mechi hiyo.

Naye mkufunzi wa Watford, Walter Mazzarri alisema, "kulikua na mazuri na ambayo si mazuri katika mechi hiyo, lakini zaidi ya yote ninajivunia timu yangu."

Leo hii kutakuwa na mechi zengine katika ligi hiyo ambapo Arsenal watakuwa wanakwaana na Sunderland walioshushwa daraja tayari, mechi hiyo ikipigwa uwanjani Emirates, halafu Manchester City wavae njuga kucheza na West Bromwich Albion.

Mwandishi: Jacob Safari/AFP/Reuters

Mhariri: Bruce Amani