GAZA: Makubaliano mapya ya kusitisha mapigano
19 Mei 2007Matangazo
Makundi hasimu ya Kipalestina,Hamas na Fatah yamekubali kusitisha mapigano ya zaidi juma moja katika Ukanda wa Gaza.Wajumbe wa makundi hayo mawili,katika mkutano uliofanywa kwenye ubalozi wa Misri mjini Gaza,walikubaliana kuwaondosha wanamgambo wao mitaani na kubadilishana mahabusu. Ni mapema mno kusema kama maafikiano hayo yatadumu,kwani makubaliano ya makundi hayo mawili kuweka chini silaha,yalivunjwa mara kwa mara.Hadi watu 50 wameuawa katika mapigano ya juma moja.