GAZA: Mateka Johnston aonyeshwa amepachikwa miripuko
26 Juni 2007Matangazo
Kanda ya video ya mwandishi wa habari wa Kingereza,Alan Johnston alietekwa nyara,Ukanda wa Gaza majuma 15 ya nyuma,imeonyeshwa kwenye mtandao wa Internet.Johnston ameonyeshwa akiwa amefungiwa miripuko mwilini na akionya kuwa kundi lililomzuia litamripua,pindi kutafanywa juhudi za kumuokoa kwa nguvu.