1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Geneva. Baraza la haki za binadamu kujadili Darfur.

13 Desemba 2006
https://p.dw.com/p/CCjl

Kikao maalum cha baraza la umoja wa mataifa la haki za binadamu kuhusiana na maafa yanayowakumba watu wa jimbo la Darfur nchini Sudan kimeahirishwa mjini Geneva hadi leo.

Katibu mkuu wa umoja wa mataifa anayemaliza muda wake Kofi Annan ametuma ujumbe kupitia video jana Jumanne, akiyataka mataifa 47 wanachama wa baraza hilo kuingilia kati katika kile alichokiita , jinamizi la Darfur kwa kupeleka wachunguzi wao binafsi.

Tangu 2003 zaidi ya watu 200,000 katika jimbo hilo wameuwawa na zaidi ya watu milioni mbili wamekimbia makaazi yao. Serikali ya Sudan inakana kuwapa silaha wanamgambo wa Janjaweed na imekuwa ikisita kukubali jeshi la nyongeza la umoja wa mataifa katika jeshi la umoja wa Afrika. Kamishna wa haki za binadamu wa umoja wa mataifa, Louise Arbour, amesema raia wanabaki kuwa lengo la mashambulizi ya kinyama kutoka kwa wanamgambo hao.