1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

GOMA : Kabila aamuru waasi kunyanganywa silaha

18 Oktoba 2007
https://p.dw.com/p/C7Eu

Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo Joseph Kabila hapo jana ameamuru vikosi vyake kujiandaa kuwanyanganya silaha wapiganaji 5,000 wa Generali muasi Laurent Nkunda.

Kabila akiwa kwenye mji mkuu wa jimbo la Kivu Kaskazini wa Goma amesema makao ya kijeshi yamepewa ruhusa kuanza kujiandaa kuwanyanganya silaha ikibidi hata kwa kutumia nguvu kwa Nkunda na wale wote walioko naye.

Kabila ameuambia mkutano wa waandishi wa habari baada ya zaidi ya mwezi mmoja wa mapambano kwenye jimbo hilo kati ya jeshi la serikali na waasi wa Nkunda kwamba Bw.Nkunda ni mhalifu na kumekuwepo hati ya kukamatwa kwake.