1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Haile Gabrselassie ashindwa kuvunja rekodi yake

18 Januari 2008
https://p.dw.com/p/CuO7

Haile Gabrselassie ameshinda mashindano ya mbio za nyika za Dubai Marathon hii leo lakini akashindwa kupata dola milioni moja kwa sekunde 30 tu.

Chipukizi huyo wa Ethiopia ameshindwa kuvunja rekodi yake mwenyewe aliyoiweka mara ya mwisho ya saa mbili dakika nne na sekunde 26 kwa kukimbia kwa muda wa saa mbili dakika nne na sekunde 53 kwa mwendo wa kilomita 42 na mita 195.

Amekimbia pamoja na wakenya Isaac Macharia na Sammy Korir, waliochukua nafasi ya pili na ya tatu.