1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Hali ya kisiasa Visiwani Zanzibar kabla ya uchaguzi mwakani

4 Agosti 2009

Zoezi la kuwaandikisha wapiga kura wepya katika daftari la kudumu la wapigaji kura kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa mwakani huko Zanzibar linakabiliana na shida.

https://p.dw.com/p/J3Xh
Rais Aman Abeid Karume wa Zanzibar.Picha: AP Photo
Watu jana na leo katika wilaya ya uchaguzi ya Ole, Kisiwani Pemba, wakisusia kujiandikisha na kupinga sharati kwamba lazima wawasilishe vitambulisho vya ukaazi wa Zanzibar kabla ya kuandikishwa. Fujo zilitokea. Leo tume ya uchaguzi huko Pemba ililazimika kusitisha zoezi hilo katika eneo hilo. Punde hivi Othman Miraji alizungumza kwa simu na mwandishi wa habari Munir Zakaria aliyekuweko katika eneo hilo na kumuomba atuarifu nini hasa kilichojiri huko Ole. Mwandishi: Othman Miraji Mhariri: Mohamed Abdulrahman