Hali ya mpakani baina ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo na Uganda
16 Agosti 2007Matangazo
Alisema jeshi la nchi yake litaitetea ardhi ya Uganda dhidi ya mtu yeyote atakayeingia nchini humo kwa nguvu. Ilitajwa hapo awali kwamba raia watatu wa Uganda na mfanyakazi wa kampuni ya Kiingereza inayochimbua mafuta katika eneo la Ziwa Albert waliuliwa na wanamgambo waliovuka mpaka kutokea Kongo.
Othman Miraji alizungumza na waziri wa habari wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, Toussent Chirombo, kutaka kujua hali ilivyo baina ya nchi hizo mbili.