1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Hamasa inapanda kuelekea uchaguzi Uturuki

Sekione Kitojo
20 Juni 2018

Kabla ya uchaguzi wa rais nchini Uturuki, mwandishi Ece Temelkuran anasifu ujasiri wa waandishi wenzake usiovunjika. Anasema ni mfano kwa wote ambao wameanza kupambana na upuuzi wa siasa kali za mrengo wa kulia.

https://p.dw.com/p/2zxCE
Türkei Wahl - Stimmungsbilder aus Diyarbakir
Picha: DW/B. Güven

Siku  chache  kabla  ya  uchaguzi ambao  rais Tayyip Erdogan amelazimisha  kuufanya  nchini  Uturuki  kujiimarisha  katika  madaraka , mjadala  mkali  katika  majukwaa  ya  kijamii unahusika  na  picha  ya mbwa  mweusi  kilema  ambaye nyayo  zake zilikatwa  na  kutupwa.

Türkei-Wahl in Deutschland
Waturuki walioko nchini Ujerumani wakipiga kura kwa ajili ya uchaguzi wa tarehe 24 mwezi Juni nchini UturukiPicha: DW/J. Danisman

Watu  wengi wameshitushwa  na  kitendo  hicho  cha  kikatili. Lakini pamoja  na  kila  kitu siku  hizi, hata  mjadala  huu  ulichukua  mtazamo wa  kisiasa. Waungaji  mkono  wa  serikali  wamepuuzia jinsi  watu walivyokuwa  wakijadili  suala  hilo  na  kusema  ni  fadhaa, wakati upinzani  umesema  ukatili  umekuwa  jambo  la  kila  siku  nchini  Uturuki baada  ya  miaka  16  ya  chama  cha  Erdogan  cha  Haki  na maendeleo AKP  kuwapo  madarakani.

Kutoka   siasa  kali  za  mrengo  wa  kulia  hadi  siasa  kali  za  mrengo wa  kushoto, watu  nchini Uturuki  wanajiweka  mbali na  mfumo  wa sasa  wa  kisiasa. Kwa  miaka  mingi, wamekuwa  wakitambua  kwamba utawala  wa  kimabavu haziishii  kwa  kupora  madaraka  ya  nchi  na kuvunja mfumo wa  kisiasa. badala  yake  zinaendelea  kushambulia na kujaribu  kuteka  nyoyo za  binadamu, kuingilia kila  sehemu  ya  maisha ya  kila  siku kwa  sumu  yake  ya  maadili yenye mabovu.

Inalazimisha  hali  ya  kutokuwa  na  sheria  na  ukatili  mkubwa  na kudai utii bila  shuruti pamoja  na  kufuata  dini kwa  viongozi  wake.

Katika  mitandao  ya  kijamii, sehemu  pekee  ambako Waturuki wanaweza  bado  kutoa  sauti  zao  na  kusikika, mjadala  halisi  sio  juu ya  mbwa  huyo  mweusi. Ni  juu  ya  nia  ya  kuendeleza  akili  timamu, kuimarisha  maadili  ya  kiutu katika  nchi  hiyo, kinyume  na  kufanywa kuwa  watu  wenye  utii tu.

Deutschland Wahllokal der türkischen General Konsulat Köln
Wagombea urais katika karatasi ya kura nchini UturukiPicha: DW/M. Karagöz

Matumaini katika uchaguzi

"Ni  matumaini  ambayo  yanachosha , sio  maumivu," niliwahi  kuandika katika  taarifa  moja. Na  maneno  haya  yamekuwa  maarufu  tena katika  mitandao  ya  kijamii. Kwasababu  watu  wa  Uturuki, kutoka  kila upande wa  uwanja  wa  kisiasa, wana  matumaini  katika  matokeo  ya uchaguzi  wa  Juni  24.

Matokeo  hayo  yanaweza  kuweka  matumaini  yao  hai kila  wakati, licha  ya  kutambua  kwamba  matokeo  ya uchaguzi  huo yataghushiwa tena,  ni  juu  ya  hamasa  na  hisia  za  upinzani, ambazo zimekuwa zikipiga  ngumi  mezani  kwa  nguvu  zaidi  kuliko  wakati  mwingine.

Mgombea  wa  chama  cha  Social Democratic Muharrem Ince, anachemka  kwa  joto  la  hamasa  katika  mikutano  yake  mikubwa, kiongozi wa  chama  cha  kizalendo , Meral Aksener, anapambana  na erdogan kwa  kutoa  hotuba  kali  kali,kiongozi  wa  chama  ambacho kwa  kiasi  kikubwa  ni  cha  wakurdi  cha  HDP , Selahattin Demirtas, ana  fanya  kampeni  akiwa  katika  chumba  chake alimofungwa  jela, ambako  amewekwa  kama mfungwa  wa  kisiasa tangu miezi  20 iliyopita.  Na  hata  chama  cha  kihafidhina  cha  Kiislamu kinazungumza lugha  ya mshikamano  dhidi  ya kutokuwa  na  haki.

Bildkombo Parteien Logos Türkei
Nembo za vyama vinavyoshiriki katika uchaguzi nchini Uturuki

Tangu  walipojiunga  pamoja  dhidi  ya  Erdogan, vyama  vyote vimekuwa  vikipambana  kana  kwamba  hakuna  kesho.  Ujumbe  wao ni  kwamba  hakuna mustakabali  wa  baadaye iwapo watapoteza uchaguzi kwa  utawala  wa  mtu  mmoja.

kuweka  matumaini  yao  juu, watu  wa  Uturuki wamevumilia  kila  aina ya  uchafu kisiasa  ambao  unaendelea  kuja  wakati  uchaguzi unakaribia. Kuvuja  kwa  picha  ya  hotuba  ya  Erdogan  katika mkutano  wa  ndani  wa  chama  chake ambako  alitoa  wito  wa kukamilisha  uchaguzi  kabla  ya  kura  kuhesabiwa, kwa  "kuweka mbinyo  katika masanduku  ya  kura".

Ripoti  za  waungaji  mkono  wa  serikali kubeba  bunduki wakati wakienda  kwa wapiga    kura  kuwaomba  wakipigia  chama  kilichoko madarakani,  katika  maeneo  ya  wakurdi. Kuwatisha  wapiga  kura  na kughushi  uchaguzi, kusambaa kwa  taarifa  za  uongo kutoka  vyombo vikuu  vya  habari, kushambuliwa  kwa  wanasiasa  wa  Kikurdi, yote hayo yanapuuziwa  na  serikali.

Mwandishi: Temelkuran, Ece  /ZR/ Sekione  Kitojo

Mhariri: Yusuf Saumu