1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

ISLAMABAD : Mvutano kwenye msikiti wapamba moto

8 Julai 2007
https://p.dw.com/p/CBko

Hali ya mvutano imezidi kuongezeka kwenye msikiti uliozingirwa katika mji mkuu wa Pakistan Islamabad kufuatia kuuwawa kwa kupigwa risasi kwa kamandoo mwandamizi wa jeshi la Pakistan na wanamgambo wa Kiislam.

Hayo ni maafa ya hivi karibuni kabisa kati ya wafuasi wa Msikiti Mwekundu na wanajeshi wa ulinzi wa Pakistan.Hapo jana Rais Pervez Musharraf amewaonya wale walijiochimbia kwenye msikiti huo kusalimu amri venginevyo watauwawa.Majeshi na magari ya deraya yamekuwa yakiuzingira msikiti huo ambao mamia ya watu wakiwemo wanawake na watoto wamejichimbia ndani tokea Jumanne.

Sheikh mkuu wa msikiti huo Abdul Rashid Ghazi na wafuasi wake wamesema wako tayari kufa mashahidi kuliko kusalimu amri.