1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

ISLAMABAD: Wapinzani wa Musharraf watawanywa kwa nguvu

29 Septemba 2007
https://p.dw.com/p/CBLi

Polisi nchini Pakistan wametumia nguvu kuvunja maandamano dhidi ya Rais Pervez Musharraf.Vikosi vya kulinda usalama,vimetumia marungu na gesi ya kutoa machozi,kutawanya makundi ya upinzani.Raia na wanasheria wanapinga kiongozi wa kijeshi Pervez Musharraf kugombea awamu nyingine. Halamashauri ya Uchaguzi lakini imethibitisha kuwa Musharraf atagombea uchaguzi wa rais uliopangwa kufanywa tarehe 6 Oktoba.