ISLAMABAD: Watu 13 wauawa Pakistan
31 Mei 2007Matangazo
Watu waliokuwa na bunduki wameivamia nyumba ya afisa mmoja mkuu wa serikali na wakawaua watu kumi na watatu katika eneo la kaskazini mashariki mwa Pakistan.
Mauaji hayo yalitekelezwa karibu na mji wa Tank katika mkoa wa Kaskazini Mashariki.
Mji wa Tank ndicho kituo cha kuingia kwenye eneo la Waziristan Kusini karibu na mpaka wa Afghanistan, eneo ambalo kuna waungaji mkono wengi wa kundi la al-Qaeda pamoja na wanamgambo wa Taliban.
Eneo hilo limekuwa lilikabiliwa mashambulio makali juma lililopita.
Polisi wa Waziristan Kusini wanachunguza sababu za shambulio hilo.