1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

ISLAMABAD:Musharraf apingana na mjumbe wa Marekani juu ya hali ya hatari

18 Novemba 2007
https://p.dw.com/p/CIm6

Naibu waziri wa mambo ya nje wa Marekani John Negroponte amemtaka rais Musharraf aondoe hali ya hatari aliyotangaza nchini Pakistan mapema mwezi huu.

Lakini jenerali Musharraf amejibu kwa kusema kwamba hali ya hatari itondolewa ikiwa usalama utaimarika nchini mwake.

Mjumbe huyo wa Marekani aliwasili nchini Pakistan siku moja baada ya kuzungumza kwa njia ya simu na kiongozi wa upinzani Benazir Bhutto alieachiwa huru ijumaa iliyopita baada ya kuzuiwa nyumbani katika mji wa Lahore.