1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Islambrotherhood-Saddam

30 Desemba 2006
https://p.dw.com/p/CCes

CAIRO:

Chama cha udugu wa kiislamu nchini Misri-Muslim Bortherhood- kimelaani kunyongwa kwa rais huyo wa zamani wa Iraq Saddam Hussein katika siku kuu ya Idd-Lhaj.Kimeeleza kuchagua siku hii ya Idd kumnyonga Saddam si-ubinadamu.Kwani ,kimesema, desturi zote zinasema siku ya leo ni siku ya kusameheana.

Waislamu kote ulimwenguni wanasherehekea siku hii yenye kukumbusha mtume Ibrahim –kwa muujibu wa Qoran,alikaribua kumtoa mhanga mwanawe- Ismail pale Mungu badala yake alipompelekea kondoo kuchinja badala yake.