1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Israel yaendelea kuitwanga Gaza

18 Aprili 2024

Israel iliendeleza mashambulizi zaidi katika Ukanda wa Gaza siku ya Alhamisi (Aprili 18), wakati mataifa yenye nguvu duniani yakihofia kuwa huenda ikaishambulia tena Iran baada ya mashambulizi ya kulipiza kisasi.

https://p.dw.com/p/4ew5W
Khan Yunis Gaza
Sehemu ya mji wa Khan Younis katika Ukanda wa Gaza.Picha: Ali Jadallah/Anadolu/picture alliance

Jeshi la Israel lilisema lilishambulia kwa mabomu maeneo kadhaa katika eneo la pwani la Palestina lenye watu milioni 2.4, miezi sita tangu ilipoanza vita vyake dhidi ya kundi la Hamas.

Mazungumzo kuhusu mapatano ya kuachiliwa huru kwa mateka waliocukuliwa na kundi la Hamas yamekwama.

Waziri Mkuu wa Qatar Mohammed bin Abdulrahman bin Jassim Al Thani alisema nchi hiyo ya Ghuba inatathmini upya jukumu lake kama mpatanishi wa mzozo huo.

Jumuiya ya kimataifa imeihimiza Israel kujizuia tangu mshambulizi ya kulipiza kisasi ya Iran dhidi ya Israel mwishoni mwa wiki iliyopita.

Soma zaidi: Israel yazidi kushinikizwa kusitisha mapigano Gaza

Mashambulizi hayo yalikuwa ni kujibu yale ya Israel kwenye ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus, Syria, ambayo yaliuwa watu kadhaa, wakiwemo majerenali wawili wa jeshi la Iran.

Miezi kadhaa ya mivutano na ghasia kubwa zinazohusisha Israel na makundi yanayoungwa mkono na Iran nchini Lebanon, Iraq, Syria na Yemen imepelekea wasiwasi wa kimataifa kwamba mgogoro wa Mashariki ya Kati huenda ukageuka vita vya eneo zima.