1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

JAKARTA: Tetemeko jipya la ardhi Indonesia

13 Septemba 2007
https://p.dw.com/p/CBQ6

Tetemeko jingine kubwa la ardhi limetokea mapema leo asubuhi katika kisiwa cha Sumatra nchini Indonesia.Tetemeko hilo lilikuwa na nguvu ya 7.8 katika Kipimo cha Richter.Saa chache kabla ya hapo,tetemeko kubwa lililotokea katika eneo hilo,liliua hadi watu 9 na kujeruhi wengi wengine na vile vile majengo mengi yaliporomoka.