1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

JAKARTA:20 wafa kutokana na mafuriko Indonesia

5 Februari 2007
https://p.dw.com/p/CCUx

Watu 20 wamekufa kutokana na mafuriko katika mji mkuu wa Indonesia, JAKARTA na watu wengine laki 3 na alfu 40 wamepoteza makao yao.

Maafisa wa nchi hiyo wamesema kuwa mafuriko makubwa kama hayo hayajawahi kutokea katika kipindi cha miaka mitano iiyopita nchini Indonesia. Maji yalifikia urefu wa mita 4 katika baadhi ya sehemu za mji.

Watabiri wa hali ya hewa wametahadhrisha kuwa mvua nyingine kubwa zinaweza kuendelea kwa muda wa wiki nzima ijayo.