JAKARTA:hali yaanza kuwa nzuri Indonesia baada ya mafuriko
8 Februari 2007Matangazo
Habari kutoka Jakarta zinasema kuwa kina cha maji kimeanza kupungua baada ya mafuriko makubwa yaliyoufunika mji huo kwa siku kadhaa.
Lakini wakaazi wa mji huo sasa wanakabiliwa na hatari ya magonjwa yanayoweza kusababishwa na maji machafu.
Watu 54 walikufa kutokana na mafuriko hayo ambayo pia yamesababisha hasara, thamani ya Euro milioni 350.